Sunday, April 13, 2025

Liwe liwalo usikate tamaa

 Changamoto ni tele maishani lakini usikate tamaa

MTU asiye na kusudi hukata tamaa haraka, mtu mwenye roho ndogo hukata tamaa upesi. Kukata tamaa ni kutokuwa na roho ya shukrani, ni kuwa mbinafsi. Kukata tamaa ni kutomwamini Mungu; anajua changamoto unazopitia, lakini bado anasema hutajaribiwa kuliko uwezo wako. Liwe liwalo usikate tamaa! Katika Luka 18, Yesu aliwaambia wanafunzi wake wamwombe Mungu kila wakati wala wasikate tamaa.


Aliwapa mfano wa kadhi asiyemcha Mungu wala kujali wanadamu, lakini mwanamke mjane alimwendea akitaka atendewe haki. Ingawaje yule kadhi alikuwa katili alilazimika kumtendea mjane aliyotaka ili asiendelee kumsumbua. Huyu mwanamke mjane alijua alichotaka, aliishi maisha yenye kusudi, alijua hatima yake ilitegemea maamuzi yake, na hakuwa tayari kukata tamaa hadi apate haki yake. Pigania haki yako kwa nguvu zako zote hata kama itakugharimu pumzi yako ya mwisho. Martin Luther King Jr. alisema, "Ikiwa mtu hajapata kitu anachostahili kufia, hafai kuishi."



Usikate tamaa maana Mungu amekutoa mbali, na ni mwaminifu kukufikisha uendako. Kumbuka alikokutoa na upate sababu ya kuendelea, kumbuka alivyokuepusha na maovu mengi maishani. Haupo salama kwa sababu wewe ni mwangalifu sana bali ni kwa rehema za Mungu. Usikate tamaa maana Mungu anakusudia kukupeleka mbali. Bado hajamalizana nawe.


Methali 23:18 inasema, “Maana bila shaka iko thawabu; na tumaini lako halitabatilika.” Usikate tamaa maana una kusudi la Mungu unalohitaji kutimiza maishani. Anakusudi kwa maisha ya kila mtu. Alimzungumuzia nabii Yeremia kuhusu kusudi lake katika Yeremia 1:5, “Kabla sijakuumba katika tumbo la mama yako nalikujua, na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.”


Usikate tamaa maana kuna watu wanakutegemea. Ukianguka, wataanguka; ukifaulu watafaulu. Katika 2 Timotheo 2:2,3 Paulo aliandika, “Mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha wengine. Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.” Usikate tamaa maana kuna mahasidi wanaosubiri tu ukate tamaa ili wafurahie. Waaibishwe, wafedheheshwe wanaoifurahia hali yako mbaya. Wavikwe aibu na fedheha wanaojikuza juu yangu (Zaburi 35:26).

Monday, March 31, 2025

All things? Yes, all things!


 

It is difficult to comprehend, but I choose to believe and trust God. Romans 8:28 says, "And we know that all things work together for good to those who love God, to those who are the called according to His purpose." (NKJV)

On 19th March 2024, after searching for 12 days, we found the body of my son, Solomon, at the mortuary. He was killed on 7th March, 21 days before his birthday.

I believed that he was going to be a great servant of God. But the Lord had other plans. I could have buried him in Machakos county where I stay, but my family prevailed upon me to take him back to my ancestral land in Rarieda, Siaya county. I said to myself, I will do annual missions in Nyilima in his memory. I want to do projects in his memory.

So I planned with our church to start this year from 3rd to 7th April. Then it dawned on me that he went to be with the Lord exactly 21 years after the first ever Flecam mission was done there. Can you imagine, during the one-day crusade, 12 people gave their lives to Jesus? Do the numbers mean anything, or am I just overthinking?

Wycliffe Otieno


The community of New Life Praise Centre is lively, cosmopolitan, familial, and energetic. We are a Bible-believing church that worships the true and living God. We believe that God still has a lot to teach us since knowing God is a continuous process and we have a lot to learn. Attendees of our fellowship are in good spirits right now, and there's a genuine feeling of excitement for what lies ahead.

In 2005, the New Life Praise Center was established. The church can be found in the Mount Kenya neighborhood at Githurai 45, close to the railway station as you head towards Kasarani Mwiki. By God's grace, Bishop Wycliffe Otieno, his spouse, and their two kids started the church. It has been an extremely challenging and exciting journey. Through divine intervention, the church has successfully developed numerous leaders and established 15 new churches throughout the nation.

Our vision is to prepare the saints for the wedding of the Lamb. Our mission is to win souls through preaching the good news of our Lord Jesus Christ, build souls in the word of God, nurture souls in the things of God, equip souls for the work of God, and send souls out for the mission of God. 

Our Leadership Team is a board usually comprised of the Senior Pastor, associate Pastors, and deacons, at present six. The Leadership Team are the trustees of the church, and are formally "responsible for the pastoral care of the members, the oversight and direction of ministry, worship, teaching, membership, fellowship, evangelism, finance, premises, all organizations and matters of policy, program and leadership".

We have been working together with the worldwide body of Christ in order to carry out our vision and missions. Every year, we have arranged both domestic and foreign conferences in addition to engaging in evangelism. The Manifast Glory Conference, which we have been hosting yearly since 2005, and the Flecam Network Conference are two of our success stories. Ministers and delegates from the United States, France, Canada, India, South Africa, Malawi, Zambia, Ghana, Togo, Nigeria, Rwanda, Burundi, Tanzania, Uganda, Congo, Angola, South Sudan, and every region of Kenya have been among the countries from which we have hosted over the years.





Additionally, we have collaborated with a number of humanitarian organizations to enhance the lives of numerous impoverished individuals and Kenyan orphanages. This includes, among other organizations, Empowering Believers Apostolic Network, Springs of Living Water Ministries, Bahari Sisters, and Kenya with Love.


The biggest need, in our opinion, is for our church members to establish connections with the neighborhood so that successful evangelism can lead newcomers to Christ. This will entail developing one's own discipleship as well as encouraging it through small group activities. We must draw in more families from the surrounding area.

Jisemee mema

 Jisemee mema, wewe ni nabii wa hatima yako

CHOCHOTE unachozungumza kujihusu hutimia. Biblia katika Methali 18:21 inasema, “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” Kila neno linalotoka kinywani mwako lina uwezo wa kukujenga au kukubomoa.

Chagua kwa makini maana wewe ni nabii wa hatima yako. Kuna mchungaji alienda kumwona mgonjwa hospitalini. Ijapokuwa aliona afya ya yule mgonjwa imeimarika sana, alipomuuliza anavyoendelea, yule mgonjwa alisema haendelei vyema.

Daktari alipoingia alimwambia yule mchungaji anamshukuru Mungu maana mgonjwa anaendelea vyema na hivi karibuni atatoka hospitalini. Lakini yule bwana alikataa na kusema madaktari ni waongo, wanasema mambo hayapo.

Watu wote waliomtembelea hospitalini walishuhudia kuwa anaendelea vyema. Lakini alipingana nao akisema anajua anaishi siku za mwisho na ameambiwa wagonjwa wengi wamefilia kwenye kitanda alichokilalia hospitalini.

Ingawaje alishuhudia kuwa hasikii uchungu mwilini, hakuamini atatoka pale akiwa hai. Baada ya siku chache alifariki. Alikuwa nabii mwenye mtazamo hasi.

Maishani kuna majira ya mambo magumu. Kuna wakati unaweza kupitia mambo mazito hadi unashuku uwepo wa Mungu.



Kuna wakati unaodhani ni marafiki wanabadilika kuwa kama wanyama. Kuna wakati unadhani mazingira ni magumu na hayakupi matumaini. Lakini hata ukiwa katika hali hiyo, unaweza kuchagua kuwa nabii wa mambo mema juu ya maisha yako. John Maxwell alisema, “Unaweza kushindwa kubadilisha mazingira yako, lakini unaweza kubadilisha mtazamo wako.” 

Endelea kujinenea maneno mazuri hata kama huoni matokeo mazuri, usikate tamaa. Maneno yako yaambatane na matarajio yako maana umeumbwa kwa mfano wa Mungu na una uwezo wa kuumba.

Hata wengine wakizungumza mabaya kukuhusu, wewe zungumza mema. Maneno yako yanajenga hatima yako. Kama vile wajenzi huwekelea tofali baada ya tofali, jiwe baada ya jiwe, kwa subira hadi nyumba ikamilike, nawe jenga kwa subira, jenga kwa ustadi, kuwa makini hadi ufikie matarajio yako.

Unahitaji mawe machache na muda mchache kujenga nyumba ndogo, lakini utahitaji mawe mengi na muda mrefu kujenga jumba kubwa. Usiwe na haraka, usishindane na mtu yeyote, hujui wanachojenga.

New Life Convention

Every 2nd week of August is set apart for the New Life annual Convention.